Karibu Kigamboni Kwa Yesu 2024 - 2031

Historia kwa ufupi

Kigamboni Kwa Yesu ni ufunuo wa miaka saba (2024-2031) ambao Mungu alimpa mtumishi wake Kamanda Dr. Peter Bujari Octoba 17, 2019. Aliandika ujumbe huo kwa mara ya kwanza kwenye ukurasa wake wa face book Octoba, 18, 2019 kuwa “Kigamboni itakuwa ufalme wa Mwanakondoo akirejea kitabu cha Zakaria 4:6.  Mwaka 2024 Juni, alirudishiwa maono wakati wa mkutano wa Injili kuwa afanye maandalizi na wakati ulikuwa umefika. Wakati huu aliambiwa kuwa uamsho unalenga kuleta miaka saba (2024-2031) ya neema na ustawi wa watu wa Kigamboni. Aliambiwa kuwa kuna madhabahu za shetani na maagano ya shetani juu ya ardhi ambayo yanapaswa kuvunjwa ili kuruhusu neema ya Mungu kuwa juu ya watu. Kwa ajili ya maagano hayo, kuna vitu vikubwa haviwezi kufanyika Kigamboni.

Maono ya Kigamboni Kwa Yesu

Nchi ambayo imejaa neem ana ustawi ambayo watu wake wanamtegemea Mungu (Jehova) na kumwamini mwanae Yesu Kristu

Utume wa Kigamboni Kwa Yesu

Kushirikisha madhehebu yote ya Kigamboni yanayoendana na kuamini katika maono ya Kigamboni Kwa Yesu kuziharibu kazi za shetani (1John 3:8) na kuruhusu mapenzi ya Mungu kutawala.

Namna ya kufikia maono: Maono haya yatafikiwa kwa:

  1. Kufanya mikutano ya injili shirikishi ndani ya Kigamboni kwa maelekezo ya Roho Mtakatifu
  2. Kufanya maombi ya mnyororo katika vipindi muhimu kutegemea na maelekezo ya Roho Mtakatifu
  3. Kufanya mikesha jumuishi kama itakavyokubalika
  4. Kufanya maombi maalmu katika maeneo mbalimbali kulingana na maelekezo ya Roho Mtakatifu

Wanufaika: Wanufaika wa uamsho huu ni watu wote wakaao Kigamboni, waingiao na kutoka kwenye malango ya Kigamboni. Litatimia lile neno la kumbukumbu 28:6 utabarikiwa uingiapo na utokapo.

Nani wajiunge: Watu wote wanaotaka kuwa sehemu ya mabadiliko ya kiroho, kuruhusu ufalme wa MUNGU kutawala Kigamboni. Wanaochukia ibada za shetani na miungu mingine

Namna ya kujiunga: Unaweza kujiunga kwa whats up HAPA. Au wasiliana nasi kwa barua pepe: kigambonikwayesu@peterbujari.com au kwa simu: 0658 536 110

MATUKIO KATIKA PICHA

kuweka msingi wa Kigamboni kwa Yesu.

Matukio yajayo
Tarehe 06-10 2024

Mkutano mkubwa wa injili KIGAMBONI

KAMATI YA KIGAMBONI
KWA YESU INAWAKARIBISHA KATIKA MKUTANO MKUBWA WA INJILI
TAREHE 06-10 NOVEMBER, 2024 I UWANJA WA KIMBUNGA, MJIMWEMA                    

Tufuatilie

#Ushindimsalabani

Scroll to Top